Muslim Brotherhood
ni nani?
Ushindi wa kihistoria wa Mohammed Mursi wa chama cha al-Ikhwan
al-Muslimun ( Muslim Brotherhood ) katika uchaguzi wa Rais wa Misri
kunabainisha mapinduzi ya vuguvugu la wanaharakati wa Kiislamu nchini humo
ambako liliasisiwa na kupigwa marufuku kwa miongo kadhaa.
Hilo ndilo vuguvugu kongwe na kubwa kabisa la Kiislamu katika
Misri;ikimaanisha kua mafunzo ya Quraan ndio msingi wa itikadi zake.
Kundi la al-Ikhwan al-Muslimun lilianzishwa na Hassan al-Banna
katika miaka ya 1920 na limeyahamasisha mavuguvugu ya harakati za kiislamu
duniani kote kwa siasa zake pamoja na shughuli zake za hisani na ufadhili wa
Kiislamu.
Mwanzoni vuguvugu hilo lilikua na lengo la kusambaza maadili ya
Kiislamu,lakini mara likajiingiza katika siasa hasa katika mapambano ya
kuungo'wa utawala wa kikoloni wa Uingereza na kuitakasa Misri na athari zote za
nchi za Magharibi.
Ingawa kundi la Ikhwan linasema linaunga mkono misingi ya
kidemokrasia moja ya malengo yake makuu ni kuunda taifa la Kiislamu
linaloongozwa na mfumo wa Sharia za kiislamu. Mojawapo wa kauli mbiu zake
inayotumika dunia nzima ni "uislamu ndio suluhisho".
Mapinduzi
Baada ya kuunda Muslim Brotherhood mnamo mwaka 1928, matawi
yalianzishwa nchini kote--kila moja likiendesha msikiti,shule na klabu cha
michezo.na wanachama wake wakaanza kukua kwa haraka.
Hassan al-Banna aliuwawa na mtu asiejulikana mnamo mwaka 1948.
Na mwishoni mwa mwongo wa 1940, inaaminiwa kikundi hicho kilikua na takriban
wafuasi millioni mbili nchini Misri na mawazo yake yalisambaa katika Baraarabu
yote.
Wakati huo huo, Banna alianzisha tawi la kijeshi lilioitwa
"zana Maalum" ambao wafuasi wake walijiunga na mapambano dhidi ya
utawala wa Uingereza na kuhusika na kampeni za mashambulizi ya mabomu na mauaji.
.
Serikali ya Misri ilikivunja kikundi hicho mwishoni mwa mwaka
1948 kwa kushambulia maslahi ya Waingereza na Mayahudi.. Muda mfupi baadae
kikundi hicho kilishtumiwa kwa kumuua Waziri Mkuu Mahmoud al-Nuqrashi.
Banna aliyalaani mauaji hayo lakini yeye mwenyewe hatimae
aliuwawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana--inaoaminiwa walikua askari
wa usalama.
Mnamo mwaka 1952, uitawala wa kikoloni ulimalizika kufuatiya
mapinduzi ya kijeshi yaliyoongozwa na kikundi cha maafisa vijana waliojiita
"Maafisa Huru".
Kundi la Ikhwan lilichangia kiasi katika mapinduzi hayo. - Anwar
al-Sadat, aliyeshika wadhifa wa Rais mnamo mwaka 1970 aliwahi kua afisa wa
uhusiano wa Maafisa Huru- na kwanza lilishirikiana na serikali mpya laini
uhusiano mara ukaharibika.
Baada ya kushindwa njama ya kumuuwa Rais Gamal Abdul Nasser
mnamo mwaka 1954, kundi la Ikhwan ndilo lilioshtumiwa kuhusika na likapigwa
marufuku na maelfu ya wafuasi wake walifungwa jela na kuteswa. Hata hicho kundi
hilo liliendelea kuimarika chini kwa chini .
Mgongano huu na serikali ulisababisha mageuzi muhimu katika
itikadi za Ikhwan, yaliobainishwa na maandishi ya mojawapo wa wafuasi wake
mashuhuri , Sayyid Qutb.
Qutb alihamasisha matumizi ya mapambano ya jihad dhidi ya jamii
"jahili" za kijinga., ziwe za nchi za Magharibi ama zinazojiita kua
za kiislamu ambazo alihoji kwamba zilihitaji mageuzi makubwa.
Maadishi yake hasa yale katika kitabu chake cha kumbukumbu
kilichochapishwa mwaka mwaka 1964 --kiliyahamasisha makundi mengi ya kiislamu
mkiwemo Islamic Jihad na al-Qaeda.
Mnamo mwaka 1965, serikali kwa mara nyingine tena ililenga
Ikhwan,ikimyonga Sayyid Qutb mnamo mwaka 1966 na kwa hiyo kumgeuza kua shujaa
katika eneo kanda nzima. .
FYEKA FYEKA
Katika miaka ya 1980 Ikhwan ilijaribu kujiunga tena katika
mkondo wa kisiasa.
Ikhwanl Muslimin -ni kundi ambalo rasmi limepigwa marufuku
ambalo mara kwa mara limejikuta likikandamizwa. Viongozi kadhaa waliunda
ushirikiano na chama cha Wafd mnamo mwaka 1984, na vyama vya Labour na Liberal
mnamo mwaka 1987,na kua nguvu kuu ya upinzani nchini Misri . Mnamo mwaka 2000,
Ikhwan ilishinda viti 17 katika bunge la wanannchi.
Miaka mitano baadae,Ikhwan ilipata matokeo bora kabisa ya
uchaguzi ,wakati wagombea wanaojitegemea wanaoshirikiana nao waliposhinda
asilimia 20 ya kura.
Matokeo haya yalimshtua sana Rais Mubarak. Serikali kisha
ikakiandama Ikhwan na kuwawekakizuizini mamia ya wafuasi wake na kutangaza
mageuzi kadha aya kisheria ili kukabiliana na muamko wa kundi hilo.
Katiba iliandikwa upya ambapo ilisisitiza kua vyama vya kisiasa
visiwe na misingi ya kidini,wagombea huru walipigwa marufuku kugombea Urais na
sheria za kupambana na ugaidi zilitangazwa ambazo zilitoa madaraka makubwa kwa
vikosi vya usalama kuweza kuwakamata washukiwa na kuekea vikwazo mikusanyiko ya
hadhara.
Viongozi wa chama tawala cha Rais Mubarak cha National
Democratic Party (NDP) pia kilifanya bidii kuvunja nguvu za wapinzani
katikauchaguzi wa bunge wa November 2010 .
Lakini juhudi zao ziligonga mwamba -baada ya madai ya njama za
kuiba kura pale ilipobainika kwamba wagombea waliofungamana na Ikhwan
hawakushinda hata kiti kimoja cha bunge.
Ikhwan kilisusia duru ya pili ya uchaguzi Novemba 2010. Kikunsi
hicho kikajiunga na vyama vingine vya upinzani katika hatua ya kususia na chama
tawala NDP kikafadhaika kwa kushinda asilimia 80 ya viti vya bunge.
Upinzani kuendelea kukandamizwa ni mojawapo wa vichocheo vikuu
vya maandamano dhidi ya serikali mnamo Januari 2011, ambapo makao makuu ya
chama tawala cha NDP mjini Cairo yaliteketezwa/.
Ikhwan ililaumiwa kwa kuchochea ghasia ,lakini naibu kiongozi
wao Mahmoud Izzat, alisisitiza kwamba yalikua mapinduzi ya umma.
Ingawa wafuasi wengi wa Ikhwan walijiunga na maandamano hayo
,walifanya hivyo bila ya kujitokeza waziwazi Medani Tahrir .
Lakini jinsi maandamano yalivyozidi kuunngwa mkono kwa wingi na
serikali kuridhia madai kadhaa mkiwemo Rais Mubarak kutogombea tena Urais ndipo
kundi hili kubwa kabisa la upinzani nchini Misri likaanza kujitutumua.
Mwanzoni mwa Februari 2011, uongozi wa Ikhwan ukatoa kauli:
"tunadai kwamba utawala huu upinduliwe na tunadai kuundwa serikali ya
muungano wa kitaifa wa makundi yote."
Halikadhalika walihudhuria mkutano ambao haujawahi kufanyika
kati ya serikali na upinzani. Mazungumzo hayo yaligeuka kua vita vya maneno
huku Ikhwan wakikataa hoja ya Makamo Rais Omar Suleiman kwamba watafute
maridhiano ,lakini mualiko huo ulikuwa ni kama wametambua kuwa kundi la Ikhwan
linaungw amkono na wengi na pia ni muhimu katika vuguvugu la maandamano.
'Halmashauri ya wanazuoni '
Umaarufu huu wa Ikhwan ulizusha upya mjadala kuhusu wangefanya
nini pindi wangeshika udhibiti wa siasa nchini Misri.
Wakosoaji wengi hasa nchini Marekani walikumbusha muongozo wa
kisiasa uliochapishwa na kundi hilo mnamo mwaka 2007, ambao ulihimiza kuundwe
halmashauri kuu ya wanazuoni kuthibitisha sheria zote zinzopitishwa na taasisi
za kiraia za Misri.Muongozo huo pia ulisema kwamba wanawake na wakristo
hawawezi kua Rais au makamo Rais.
Hata wafuasi wenye msimamo wa wastani hawakukubaliana na
muongozo huo ingawa wakereketwa walisistiza kwamba katiba inasema waziwazi
kwamba Uislamu nduio dini ya taifa na sharia za kiislamu ndio msingi wa sheria
kuu nchini.
Ni wazi kwamba viongozi wa Ikhwan wamejitolea kuimarisha hadhi
ya Uislamu katika maisha ya wananchi wa Misri ,na kuuweka zaidi mfumo wa Shariah
katikati ya sera za taifa.
Lakini mjumbe mwaandamizi wa Ikhwan, Issam al-Aryan, ameiambia
BBC kwamba wanataka "taifa la raia kwa mujibu wa misingi ya
kiislamu". Taifa la kidemokrasia,lenye mfumo wa bunge ,lenye uhuru wa
kuunda vyama,uhuru wa vyombo vya habari na mahakama huru na za haki.
Taarifa
zinazohusiana
No comments:
Post a Comment